Mwanamitindo Flaviana Matata Akabidhi Madarasa Mawili Shule ya Msingi Msinune


Na Evance Ng'ingo

MWANAMITINDO wa kimataifa afanyaye shughuli zake nchini Marekani, Flaviana Matata madarasa mawili ya shule za msingi iliyopo katika kijiji cha Msinune kilichopo kata ya Kiwangwa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

Flaviana alipewa jukumu la ulezi wa shule hiyo na wanakijiji wa Msinune mwaka 2014 wakati alipoenda kuwasaidia wanafunzi mabegi ya shule, walimpatia jukumu la kuwatengenezea vyoo, ofisi na nyumba za walimu pamoja na kumalizia ujenzi wa darasa.

Tangia alipopewa majukumu hayo alianza kwa ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi, na juzi alienda kukabidhi jengo la madarasa, darasa la saba na la sita pamoja na ofisi ya Mkuu wa Shule.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Flaviana alisema, tangia alipopewa jukumu la ulezi wa shule hiyo amekuwa akihangaika huku na kule kupata fedha za kutatua kero za shule hiyo.
Alisema, kwa kufanikiwa kukabidhi jengo hio la madarasa anaona kuwa ameshiriki kikamilifu katika kutekeleza jukumu lake kama mwanajamii la kusaidia maendeleo ya elimu kwa jamii iliyokuwa na uhitaji mkubwa.

Alisema" sisi kama vijana kama watanzania tunalo jukumu la kujitokeza na kusaidia maendeleo ya elimu na sekta nyingine muhimu nchini kwa kuwa hili sio jukumu la serikali peke yake, sasa nimeshatengeneza vyoo vya walimu na wanafunzi na leo nakabidhi darasa"

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Alex Lugaigalila alisema ujenzi wa darasa huo utawaongezea ufanisi wanafunzi katika masomo yao huku akibainisha wazi ushiriki wa Flaviana kwenye maendeleo ya shule hiyo umeongeza hamasa ya wanafunzi kusoma.

Kwa upande wake Afisa wa elimu wa Kata hiyo,Blasius Alphonce alisema kwa ujenzi wa jengo hilo, Flaviana amesaidia jitihada za serikali katika kuendeleza elimu kwenye kata hiyo yenye vijiji vitano.
Jengo hilo la darasa lililojengwa lina vyumba viwili vikubwa vilivyoezekwa kwa bati huku likuwa na madirisha makubwa yanayowezesha kupitisha hewa na chumba cha mwalimu mkuu.
 

0 comments:

Post a Comment